Serikali imefunga vyuo vyake saba kutokana na wanafunzi kugoma kuingia madarasani wakishinikiza sera ya uchangiaji elimu ibadilishwe na kama itaendelea, basi wanafunzi wakopeshwe kwa asilimia mia badala ya mpango wa sasa (means testing) ambao huchambua uwezo wa familia ya mwanafunzi na kuwapanga kwa makundi.
Vyuo vilivyofungwa ni Chuo Kikuu cha Dar es salaam (UDSM), Chuo Kikuu Kishiriki cha Ualimu (Duce), Chuo Kikuu cha Ushirika na Biashara (MUCCOBS), Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine, Chuo Kikuu Kishiriki cha Ardhi, Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Mkwawa na Taasisi ya Teknolojia ya Dar es salaam (DIT).
No comments:
Post a Comment