Tuesday, November 25, 2008

Sakata la migomo Vyuo vikuu na Kauli ya Rais

Kauli ya Rais Jakaya Kikwete kuwa serikali yake haikubaliani na matakwa ya wanafunzi kudai wakopeshwe asilimia 100 ya gharama za masomo, imepokelewa kwa hisia tofauti na wanasiasa wakieleza kuwa kwa msimamo huo taifa linaelekea gizani na kwamba athari zake hazitakawia.

Serikali imefunga vyuo vyake saba kutokana na wanafunzi kugoma kuingia madarasani wakishinikiza sera ya uchangiaji elimu ibadilishwe na kama itaendelea, basi wanafunzi wakopeshwe kwa asilimia mia badala ya mpango wa sasa (means testing) ambao huchambua uwezo wa familia ya mwanafunzi na kuwapanga kwa makundi.

Vyuo vilivyofungwa ni Chuo Kikuu cha Dar es salaam (UDSM), Chuo Kikuu Kishiriki cha Ualimu (Duce), Chuo Kikuu cha Ushirika na Biashara (MUCCOBS), Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine, Chuo Kikuu Kishiriki cha Ardhi, Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Mkwawa na Taasisi ya Teknolojia ya Dar es salaam (DIT).

Tembelea hapa

No comments: