Wednesday, October 29, 2008

Tafrani la wana Jumuiya ya Afrika Mashariki..

Baadhi ya wakazi wa Jijini, wakishindwa kuvuka kuja mjini leo asbh kutokana na Wazee wa iliyokuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki kuziba barabara ya Ali Hassan Mwinyi katika eneo la Salender Bridge leo Asbh..

Wastaafu wa iliyokuwa East Africa Community (Jumuiya ya Afrika Mashariki) leo alfajiri majira ya saa 1:00, walijitokeza na kufunga barabara ya Ali hassan Mwinyi eneo la daraja la Salender katika kuishinika serikali iweze kuwalipa mafao yao, Wazee hao baadhi walikuwa wanapiga mayowe, wengine walionekana wakisali na hata wengine walisaula viwalo vyao katika kuonyesha machungu waliyonayo kutokana na kutolipwa viinua mgongo vyao kwa kipindi kirefu. Tukio hilo liliweza kushuhudiwa na Mkuu wa mkoa wa dar es salaam Bw. Abass Kandoro, na Kamanda wa kikosi cha kanda maalum Bw. Suleiman Kova..

No comments: