
Ambwene Yessayah. Maarufu kama 'A.Y' huku wengine wakimuita “Mzee wa Commercial”. Mafanikio yake katika muziki ni mfano wa kuigwa na wengi hasa kwa wasanii chipukizi, A.Y ni miongoni mwa wawakilishi wazuri wa Tanzania nje ya nchi kupitia sanaa ya muziki. Kwa mara nyingine tena mwaka huu anawania tuzo maarufu za Kisima za nchini Kenya.
Kwa sasa jamaa anatamba na kibao kinachoenda kwa jina la 'Freeze' akiwa ameshirikiana na wakali 'P Square' wazee wa 'Do me' kutoka nchini Nigeria. Wimbo umetayarishwa na kurekodiwa na Producer 'Hermy B' kutoka Tanzania, na kuna tetesi kuwa video yake inatarajiwa kufanyika nchini Nigeria na baadhi ya nchi nyingine za Afrika ikiwemo Tanzania. Tayari wimbo huu unakamata chart katika vituo mbalimbali vya radio hapa nchini na huko Nigeria..
Kwa sasa jamaa anatamba na kibao kinachoenda kwa jina la 'Freeze' akiwa ameshirikiana na wakali 'P Square' wazee wa 'Do me' kutoka nchini Nigeria. Wimbo umetayarishwa na kurekodiwa na Producer 'Hermy B' kutoka Tanzania, na kuna tetesi kuwa video yake inatarajiwa kufanyika nchini Nigeria na baadhi ya nchi nyingine za Afrika ikiwemo Tanzania. Tayari wimbo huu unakamata chart katika vituo mbalimbali vya radio hapa nchini na huko Nigeria..
1 comment:
Jamaa yuko juu sana, Bigup mwenetu kaza msuli jibaba..
Francis, Dar
Post a Comment