Friday, October 31, 2008
Mrithi wa Chacha Wangwe Aapishwa Bungeni
Thursday, October 30, 2008
Ni wakati wa ku-Freeze

Kwa sasa jamaa anatamba na kibao kinachoenda kwa jina la 'Freeze' akiwa ameshirikiana na wakali 'P Square' wazee wa 'Do me' kutoka nchini Nigeria. Wimbo umetayarishwa na kurekodiwa na Producer 'Hermy B' kutoka Tanzania, na kuna tetesi kuwa video yake inatarajiwa kufanyika nchini Nigeria na baadhi ya nchi nyingine za Afrika ikiwemo Tanzania. Tayari wimbo huu unakamata chart katika vituo mbalimbali vya radio hapa nchini na huko Nigeria..
Wednesday, October 29, 2008
Tafrani la wana Jumuiya ya Afrika Mashariki..


Nyamaza...

Pantoni lakwama Dar..

Fiesta Jirambe ndani ya Dom
Tigo na Xtreme Party
Wahariri waandamana Dar

Monday, October 27, 2008
Mnyama Simba apigwa Moja
Sunday, October 26, 2008
KLM wazindua Boeing 777

Shirika la Ndege la KLM la uholanzi, leo linatambulisha yake ndege aina ya Boeing 777 inayotarajiwa kutua usiku huu tayari kwa kuanza safari zake kupitia Dar, utambulisho huu umepambwa na kikundi cha ngoma cha Steel of Heaven (Mapipa ya Mbinguni) cha Kurasini kilichoonyesha umahiri wa kupiga nyimbo mbalimbali maarufu hapa nchini wakitumia mapipa.. Pichani ni mfano wa ndege hiyo ambayo imeshatambulishwa nchi nyingi za bara Ulaya, Sherehe hizo zilifanyika katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere (JNIA)
Rudy Ray Moore Afariki Dunia

Mungu ailaze Roho Rudy mahali pema peponi... Amen
Prezzo akimpigia debe 'Obama' kiaina..

'College Bash' ilivyopagawisha
Mambo ya Fiesta 'Jirambe'


Pichani ni wasanii wa Nyumba ya Vipaji Tanzania maarufu kama THT au kwa kirefu Tanzania House of Talent wakiwa jukwaani kwenye tamasha la Fiesta Jirambe 2008.
Msafara wa Fiesta Jirambe Moro

JK ahani msiba wa Watoto Tabora
Rais Jakaya Mrisho Kikwete jana amekutana na kuwapa pole binafsi wananchi wa mjini Tabora, ambao mwanzoni mwa mwezi huu walifiwa na watoto wao 19 katika tukio la kusikitisha kwenye Sikukuu ya Idd El Fitr, Oktoba Mosi, mwaka huu.
Rais, ambaye ameanza ziara ya kikazi ya siku nane ya mkoa huo, amekutana na wazazi na walezi 16 wa watoto hao waliopoteza maisha kwenye ajali ya kubanana kwenye ukumbi wa disco wakati ulipotokea moto kwenye ukumbi huo kwenye jengo la NSSF mjini Tabora.
Watoto wengine 16 walilazwa hospitali kutokana na kuumia katika tukio
Baada ya kuwa amempa mkono kila mfiwa katika tukio
“Siku ile ya Idd El Fitr, nilipata habari za kusikitisha za msiba wa watoto wetu. Nikamtuma Waziri Kapuya (Profesa Juma Athuman Kapuya – Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana) kuja kuungana nanyi kwa niaba ya Serikali kwenye msiba huu. Lakini maadamu nimepata nafasi ya kuja hapa mwenyewe, nimeona ni jambo zuri nikutane, ili niweze kuwapeni pole mimi binafsi.
Ameongeza Rais: “Nataka mjue kuwa msiba wenu, ni msiba wetu sote. Majonzi yenu, ni majonzi yetu, Masikitiko yenu, ni masikitiko yetu. Kila mzazi hupenda mtoto wake aweze kukua na kumzika yeye. Lakini pia Mwenyezi Mungu ana mipango na maamuzi yake. Nawapeni pole na kuwafariji wa namna ya pekee.”
Wazazi hao nao wamemshukuru Rais Kikwete binafsi, na uongozi wa wilaya ya Tabora na mkoa wa Tabora kwa namna ya pekee ambayo walishiriki katika kuwafariji wakati wa msiba huo mkubwa.
Mara baada ya kutokea ajali na msiba huo, Rais alitoa ubani wa sh 500,000 kwa kila mototo aliyepoteza maisha na sh 100,000 kwa kila mtoto aliyeumia.
Miongoni mwa watu wengine ambao walitoa ubani ni mke wa Rais, Mama Salma Kikwete, na Mbunge wa Igunga, mkoani Tabora, Rostam Aziz.
Ngeleja akabidhi mradi wa Umeme Salasala

Waziri wa Nishati na Madini Mh. William Ngeleja amekabidhi Mradi wa umeme uliopo kijiji cha Salasala uliojengwa chini ya mradi wa uendelezaji wa gesi ya asili ya Songosongo sherehe hiyo iliambatana na kukabidhi miradi mingine waliyoijenga ambayo ni maji, barabara na simu, katika maeneo ya Salasala na Kinyerezi. Hafla hiyo ilifanyika maeneo ya Salasala nje kidogo ya jiji la Dar, Aidha Wilaya hiyo imejengewa barabara tano za lami zenye urefu wa kilomita sita na nusu.
Odemba kurudisha Heshima?

Mrembo Miriam Odemba kwa mara nyengine tena amekabidhiwa bendera ya nchi akiwa kama Miss Earth Tanzania, baada ya kuharibu ile ya Face of Tanzania, je ataweza rudisha heshima kama ile tena? Miriam ambaye ni mzoefu katika masuala ya uanamitindo ameanza mashindano ya Miss Earth, Phillipines ambapo ameweza kuwa kivutio kikubwa kwa wananchi wa pale. Hivi karibuni, Miriam aliungana na washiriki wenzake katika maonyesho ya mavazi yaliyofanyika katika jengo la duka la Robinson Mall. Miriam hivi sasa anatabiriwa na wataalamu wengi kufanya vizuri katika mashindano hayo kutokana na kile walichosema ni mvuto wa sura, uwezo wa kutembea jukwaani na kujiamini katika mahojiano na vyombo vya habari. "Tanzania imetoa mrembo ambaye ameonyesha umahiri mkubwa" aliandika Marco Ramirez ambaye ni mtaalamu wa masuala ya urembo Philippines. "Huyu (Miriam Odemba) amenishtua sana. Ni mshiriki ambaye ni mmoja wa washiriki washindani wa kunyakua taji. Uchangamfu wake ndio unanifanya nimpe nafasi.” Mashindano ya Miss Earth yatafikia kilele tarehe 9 Novemba huko Manila, Phillipines ambapo warembo 93 watawania taji la Miss Earth na mataji mengine. Miss Earth pia ina mashindano mengine madogo yanayomwezesha mshiriki kujizolea umaarufu na zawadi ndogondogo kama taji la vazi la ufukweni, kipaji na nguo ya jioni
Wateule wajipanga Upya

Yawezekana kuwa si jambo lililotarajiwa kutokea ktk siku za karibuni,lakini ukweli ni kwamba kundi la 'Wateule' linarejea upyaaaa....na tayari memba waliokuwa wakiunda kundi hilo tayari wamemesharekodi nyimbo nne. Unaweza usiamini kinachotokea lakini Jahffarai ambaye alikuwa akiongea kwa niaba ya wenzake anasema.... "Pini ambazo tumesharekodi hadi hivi sasa ni 'Tumetoka Mbali`, `Msela`, `Bado Yuko Vilevile` na `Mtaani Kuna Njaa`.....na albam inakuja,`` . Rapa huyo alisema ufufuko huo wa Wateule unahusisha muungano mpya wa memba wa kundi hilo - Jaymoe, Mchizi Mox, Kevin Kimali, yeye mwenyewe Jaffarai na Solo Thang ambaye kwa sasa anaishi Uingereza. .....``Katika pini hizi za kwanza tumerekodi sisi wanne bila ya kumshirikisha Solo Thang, lakini mipango inafanywa ili kumtumia beats ili atie mistari yake katika nyimbo zinazofuata. ``Marejeo haya ni `sirias` na tunatarajia kuwashirikisha wakali wa Afrika Mashariki kwa kuwa lengo letu sasa ni kusonga mbele.`` ``Ninapokwambia kuwa marejeo haya ni `sirias` ni kwamba ninamaanisha hivyo, wakati wowote tutaanza kurekodi video yetu ya kwanza ya wimbo wa `Mtaani Kuna Njaa` na muda mfupi baadaye tutaachia pini la kwanza la utambulisho katika vituo vya radio,`` alisema Jaffarai. ``Tumeungana kufanya kazi pamoja kwa mara nyingine kwakuwa tunafahamu nguvu kubwa iliyokuwepo ya kundi letu kabla ya kumeguka. Nadhani unaweza kuwa na japo picha ya nini kitatokea vinapokaa vichwa hivi pamoja,`` alisema. Kuungana upya kwa memba wa Wateule kunaashiria jambo. MWAKA WA MALAIKA? Pengine `mwaka wa shetani` ulioimbwa na rapa wa TMK Wanaume Family Mheshimiwa Temba baada ya kushuhudia makundi kibao yakivunjika umefikia tamati. Pengine TMK Wanaume Family na Wanaume Halisi nao wataungana upya mwaka huu, au MwanaFA na AY watarejea kwa kamanda wao wa zamani King Crazy GK wa EastCoast Team. Au Ferooz na Daz Baba wataungana tena kuliteremsha upya majini jahazi lao la Daz Nundaz. Nani ajuaye ya kesho? Lakini kuungana upya kwa Wateule, bila ya shaka, ni jambo ambalo lilikuwa likisubiriwa kwa hamu na mashabiki wa hip hop kwasababu wanajua. Wanajua nini wanachotarajia kutoka kwa wakali hao wa mistari waliotambulishwa katika gemu mwaka 2000 kupitia wimbo wao wa ?Hip Hop na Ragga?. WATU KIBAO Wimbo wa `Hip Hop na Ragga` ulikuwa ni kazi ya kwanza na ya mwisho kubwa kwa kundi hilo ambalo liliundwa baada ya wakali hao kukutana kwa mtayarishaji wa muziki P-Funk kwa lengo la kurekodi nyimbo - kila mtu wa kwake - kufuatia ofa waliyopata baada ya kushinda mashindano ya vipaji vya muziki ya Pilsner Ice Pop Stars 2000. Kundi la Sower Cellibas lililoundwa na Jaymoe, Mchizi Mox na Kevin Kimali lilikuwa limeshinda katika kategori ya hip hop, na Solo Thang aliibuka wa pili baada ya kuyapiku makundi na wasanii mbalimbali kama HBC, BDP na Inspektah Haroun. Mark II B alikuwa wa kwanza katika kategori ya Ragga akifuatiwa na Lady Lou, katika mashindano hayo yaliyofanyika kwenye ukumbi wa Mambo Club. ``Ushindi wa kila msanii ama kundi ulitupatia nafasi ya kurekodi wimbo katika studio ya Bongo Records,`` anakumbuka Jaffarai. ``Lakini tukiwa pale studio kwa ajili ya kurekodi wimbo kwa kila mshindi, prodyuza P-Funk alionekana kama kuingia hofu kama tutaweza kufanya vizuri kama kila mmoja atarekodi kivyake, akatushauri turekodi pamoja. ``Kwa sababu ulikuwa ni muunganiko wa wasanii wa hip hop na wa ragga, tukaamua kuuita wimbo huo ?Hip Hop na Ragga`. ``Baada ya kurekodi na prodyuza kukubali kuwa `pini` limetulia, alitushauri tutafute jina na tuendelee kufanya kazi pamoja. ``Wakati tukijiuliza tutumie jina gani, ndipo Kevin Kimali alipotoka na jina hili la Wateule akimaanisha washindi baada ya shindano la pop stars. ``Kundi likaundwa na wasanii saba Mchizi Mox, Kimali, Solo Thang, Jaymoe, Lady Lou, Mark II B na mimi (Jaffarai).`` Muda mfupi baadaye, Solo Thang akajitoa ili afanye kazi kivyake, akifuatiwa na Jaymoe, Lady Lou na Mark II B na kuwaacha wasanii watatu - Mox, Jaffarai na Kimali - ambao wakarekodi katika studio ya MJ Records nyimbo za `Nipende Nichukie`, na ?Watu Kibao? iliyowatoa kiukweli. Katika marejeo, Wateule hawajasahau njia walizopitia awali. Ndiyo maana wamerekodi kwa MJ na pia kwa P-Funk. ``Na tuna nyimbo tutazirekodi nchini Kenya na Uganda,`` alisema Jaffarai. Hata hivyo Jahffarai anasema kurejea kwao hakutawashirikisha wenzao wawili Lady Lou na Mark II B...ambao wao wameamua kukaa mbali na muziki kwa miaka mingi sasa.
Tanzania Information and History
Tanzania, the largest country in East Africa, includes the spice islands of Zanzibar, Pemba, and Mafia and contains Africa's highest point—Kilimanjaro, at 5,895 meters (19,340 feet). Kilimanjaro, a dormant volcano, is snowcapped even though it is near the Equator. The African population consists of more than 120 ethnic groups.
Tanganyika, a British-controlled UN trust territory, gained independence in 1961; and Zanzibar, a British protectorate with an Arab population, became independent in 1963. Tanganyika and Zanzibar united to form Tanzania in 1964. Until resigning as president in 1985, independence leader Julius K. Nyerere guided two decades of socialism—adapted to the ujamaa policy of village farming. A multiparty system was established in 1992 after a constitutional amendment.
Some 80 percent of Tanzanians farm or fish at subsistence levels; in many areas tse-tse fly infestation hampers successful animal husbandry. Deteriorating roads and railways and high energy costs are major problems. The Ngorongoro Crater and Serengeti National Park are rich in wildlife, although poaching endangers some species. Tourism remains important. Dar es Salaam is the administrative capital, but Dodoma is the designated future capital and current home to Tanzania's legislature.
ECONOMY Industry: agricultural processing (sugar, beer, cigarettes, sisal twine), diamond and gold mining, oil refining. Agriculture: coffee, sisal, tea, cotton; cattle. Exports: gold, coffee, cashew nuts, manufactures, cotton.